Ihefu F.C. ni klabu ya mpira wa miguu ya nchini Tanzania iliyopo mkoani Mbeya. Makao makuu ya klabu hiyo ni Wilaya ya Mbarali kata ya Ubaruku ambapo ndipo ulipo uwanja wa klabu hii.
Kwa sasa michezo yao ya nyumbani inachezwa kwenye Uwanja wa Highlands Estates Stadium, uliopo Ubaruku wilayani Mbarali, mkoa wa Mbeya.